https://youtube.com/shorts/w6syhZxAkH4?feature=share
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Masasi Mjini, Dkt. Leonard Akwilapo, ameonyesha mfano wa namna sahihi ya kupiga tiki kwenye karatasi ya nafasi ya Urais, akionyesha wazi alama ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na picha ya mgombea urais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Zoezi hilo lililofanyika wakati wa mkutano wa kampeni limekuwa sehemu ya elimu endelevu ya kuhakikisha wananchi wanapiga kura kwa usahihi ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025, kwa kutiki sehemu husika katika karatasi ya kura na kuhakikisha kura zote zinaenda kwa CCM
kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge hadi Udiwani.